Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2015

HOTUBA YA JOHN POMBE MAGUFULI - MGOMBEA URAIS CCM

Ifuatayo ni hotuba ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli, mgombea wa CCM kwa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akitambulishwa rasmi mjini Dodoma, tarehe 12 Julai 2015.  Awali ya yote, napenda nichukue fursa hii adhimu sana, kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote yaliyofanyika hata kuniwezesha leo hii kuwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi. Namshukuru kwanza, kwa kutufikisha wote hapa tukiwa buheri wa afya. Namshukuru pia, kwa kutusimamia vizuri, kwa Usalama na Amani toka kuanza kwa mchakato huu hadi hapa tulipofikia. Tunazidi kumuomba aendelee kutusimamia mpaka ushindi utakapopatikana. John Pombe Magufuli na Jakaya M. Kikwete Naomba nirudie tena kuwashukuru kwa moyo wa dhati Kamati Kuu, Wajumbe wa Halmashauri Kuu na Wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa heshima kubwa mliyonipa kuipeperusha bendera ya CCM katika kinyang’aniro cha Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015. Nakosa maneno sahihi na muafaka ya kuwashukuru. Ahadi yangu kwenu ni kwamba sitowaan

HOTUBA YA JOHN POMBE MAGUFULI - MGOMBEA URAIS CCM

Ifuatayo ni hotuba ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli, mgombea wa CCM kwa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akitambulishwa rasmi mjini Dodoma, tarehe 12 Julai 2015.  Awali ya yote, napenda nichukue fursa hii adhimu sana, kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote yaliyofanyika hata kuniwezesha leo hii kuwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi. Namshukuru kwanza, kwa kutufikisha wote hapa tukiwa buheri wa afya. Namshukuru pia, kwa kutusimamia vizuri, kwa Usalama na Amani toka kuanza kwa mchakato huu hadi hapa tulipofikia. Tunazidi kumuomba aendelee kutusimamia mpaka ushindi utakapopatikana. John Pombe Magufuli na Jakaya M. Kikwete Naomba nirudie tena kuwashukuru kwa moyo wa dhati Kamati Kuu, Wajumbe wa Halmashauri Kuu na Wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa heshima kubwa mliyonipa kuipeperusha bendera ya CCM katika kinyang’aniro cha Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015. Nakosa maneno sahihi na muafaka ya kuwashukuru. Ahadi yangu kwenu ni kwamba s